Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ameshiriki Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Botswana, Hayati Festus Gontebanye Mogae, yaliyofanyika jijini Gaborone. Mheshimiwa Dkt. Kikwete amemwakilisha Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Katika mazishi hayo Mheshimiwa Dkt. Kikwete alimbatana na Mhe.Balozi James G.Bwana, Balozi wa Tanzania nchini Botswana, mwenye Makazi yake nchini Afrika Kusini.
Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Kikwete amesema Tanzania inaungana na Serikali pamoja na Wananchi wa Botswana katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo. Alisema kuwa wakati wa uongozi wa Hayati Mogae, ushirikiano na uhusiano wa kindugu kati ya Tanzania na Botswana uliendelea kuimarika kwa kiwango kikubwa. "Hayati Rais Mogae alikuwa rafiki wa kweli wa Tanzania na alipenda nchi yetu kwa dhati," alisema Dkt. Kikwete.
Akizungumzia uhusiano wake binafsi na Hayati Mogae, Dkt. Kikwete aliongeza: "Nilipata heshima ya kufanya kazi naye alipokuwa Makamu wa Rais, wakati mimi nikihudumu kama Waziri. Alikuwa mtu mzuri kufanya naye kazi, mwenye misimamo, mwadilifu, na siku zote alikuwa akisema kilealichokiamini, lakini kwa upole na heshima." Mazishi hayo ya Kitaifa yalihudhuriwa na Raia wa Botswana, Wakuu wa Nchi na Serikali, Viongozi Wastaatu kutoka Nchi za Afrika, Mabalozi na Wawakilishi wa Taasisi za Kimataifa.